Sunday, July 1, 2012
MKURUGENZI WA CRDB AFUNGUA TAWI JIPYA TEGETA
Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB Dk Charles Kimei akikata utepe kuzindua tawi jipya la benki hiyo Tegeta jijini Dar es Salaam
WATOTO WAPEWA MATONE YA VITAMINI A
Mmoja wa watoto waliopelekwa kupimwa afya zao katika hospitali ya TMJ jijini Dar es Salaam wakipatiwa dawa ya vitamini A na Mganga Mkuu wa wilaya ya Kinondoni Dk Gunini Kamba
WAZIRI WA NISHATI NA UMEME AZINDUA MTAMBO WA UMEME
Waziri wa Nishati na Madini, Prof Sospeter Muhongo akiwa katika mtambo wa umeme unaotumia gesi asilia Ubungo kabla ya kuuzindua
Saturday, June 30, 2012
GARI LA WAGONJWA LILILOMBEBA DK ULIMBOKA LIKIINGIA KATIKA UWANJA WA NDEGE
Gari la wagonjwa lililombeba Dk Ulimboka likiingia katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam tayari kusafirishwa kupelekwa nje ya nchi kwa matibabu.
WANAHARAKATI WAKIWA WAMESHIKA MABANGO YENYE UJUMBE MBALIMBALI KUMUAGA DK ULIMBOKA ANAYEPEKWA NJE YA NCHI KWA MATIBABU
Baadhi ya wanaharakati na madaktari wakiwa wamebeba mabango yenye ujumbe wa aina mbalimbali kumuaga Dokta Stephen Ulimboka ambaye alisafirishwa nje ya nchi kwa matibabu zaidi kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam
Monday, June 25, 2012
ASKARI WA KIKOSI CHA KUTULIZA GHASIA WAKIULINDAMWENGE MARA BAADA YA KUINGIA JIJINI DAR ES SALAAM
Askari kutoka jeshi la
Polisi wakiimarisha ulinzi wakati wa sherehe za mapokezi ya Mwenge wa Uhuru leo
jijini Dar es Salaam.Picha: Aron Msigwa -
MAELEZO
MKUU WA MKOA WA DAR ES SALAAM APOKEA MWENGE
Mkuu wa mkoa wa Dar
es Salam Saidi Meck Sadik (kulia) akipokea mwenge wa Uhuru kutoka kwa
mmoja wa wakimbiza Mwenge wa Uhuru Kitaifa Bi. Tatu Saidi Mussa leo jijini Dar es Salaam . Mwenge wa
Uhuru umewasili jijini Dar es Salaam
ukitokea Mkoa wa Kusini Pemba.
WAKIMBIZA WAKIELEKEA KUANZA MBIO HIZO WILAYANI TEMEKE
Wakimbiza Mwenge
kitaifa wakiongozwa na kiongozi wa mbio za Mwenge Capt. Ernest Mwanossa (wa
kwanza mbele) wakianza safari kuelekea maeneo mbalimbali ya wilaya ya
Temeke leo jijini Dar es Salaam.
MWENGE WA UHURU WAINGIA DAR
Mkuu wa wilaya ya
Temeke Bi. Sophia Mjema akiahidi mbele ya mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Saidi
Meck Sadik kuupokea Mwenge wa Uhuru na kuukimbiza katika maeneo mbalimbali ya
wilaya hiyo ambapo miradi 11 itafunguliwa na kuwekewa mawe ya msingi.
AIRTEL NA SUPA 5
Ni Mzee wa Makamo hivi lakini alionesha umahiri wake mkubwa wa
kuwachangamsha vilivyo sehemu ya wakazi wa jiji la Mwanza.Anaitwa Mzee
Salum akikamua jukwaani jana kwenye viwanja vya Furahisha jijini
Mwanza,wakati wa uzinduzi wa huduma mpya ya Airtel Jiunge na Supa5.
Subscribe to:
Comments (Atom)
